Kurasa.
MapenziKiswahiliDakika 5👁 7,151Sehemu 1 ya 10

# KIVULI CHA UMASKINI

Na BARAKA · 12 Julai 2026

📖

Hadithi ya bure 1 kati ya 3 · Jiunge usome bila kikomo.

Sura ya Kwanza: Mvua ya Bahati

Kijiji cha Mlimani kilikuwa kimetulia kama kawaida. Jua lilikuwa linazama taratibu huku upepo ukivuma juu ya mashamba ya mahindi yaliyokuwa yameanza kukauka. Katika kijiji hicho aliishi kijana mmoja aliyeitwa Daniel.

Daniel alikuwa na miaka ishirini na tano.

Hakuwahi kumjua baba yake. Alilelewa na mama yake mzazi aliyekuwa akifanya vibarua vya kufua nguo za watu na kulima mashamba ya wengine ili wapate chakula cha siku. Mara nyingi walilala njaa. Kulikuwa na siku ambazo waligawana embe moja na kulifanya chakula cha usiku.

Licha ya maisha hayo magumu, Daniel alikuwa na tabia ya kipekee.

Hakuwahi kuiba.

Hakuwahi kudanganya.

Hakuwahi kulalamika.

Alikuwa akiamini kuwa siku moja Mungu angebadilisha maisha yake.

Siku moja mama yake aliugua ghafla.

"Dani..." mama yake alisema kwa sauti dhaifu.

"Ndio mama."

"Usije ukakata tamaa kwa sababu ya umaskini."

Daniel alilia kimya kimya.

Wiki mbili baadaye mama yake alifariki.

Alibaki peke yake duniani.

Baada ya mazishi, hakukuwa na nyumba, hakukuwa na shamba, hakukuwa na ndugu wa kumsaidia.

Alianza kutafuta kazi popote.

Baada ya wiki kadhaa, alipewa kazi katika familia ya tajiri mkubwa wa eneo hilo, Mzee Richard Mwakalinga.


Shiriki:

Zaidi katika Mapenzi

Maoni

💬

Maoni ni kwa wanachama

Jiunge na Kurasa ili uweze kushiriki mawazo yako na kujadili hadithi pamoja na wasomaji wengine.

Fungua akaunti

Tayari una akaunti? Ingia

Bado hakuna maoni. Kuwa wa kwanza kuandika!