# KIVULI CHA UMASKINI
Na BARAKA · 12 Julai 2026
Sura ya Pili: Binti wa Tajiri
Mzee Richard alikuwa mfanyabiashara mkubwa sana.
Alimiliki mashamba, maghala, magari mengi na kampuni kadhaa.
Lakini alikuwa na mtoto mmoja tu.
Jina lake lilikuwa Eliana.
Eliana alikuwa na miaka ishirini na tatu.
Alikuwa amemaliza masomo yake katika chuo kikuu nje ya mji na alikuwa amerudi nyumbani kwa likizo ndefu kabla ya kuanza kazi katika kampuni ya baba yake.
Alipofika nyumbani, macho yake yalikutana kwa mara ya kwanza na Daniel aliyekuwa akipanda maua bustanini.
Daniel alikuwa ameinama akipalilia maua.
Uso wake ulikuwa umejaa jasho.
Mikono yake ilikuwa imejaa udongo.
Lakini tabasamu lake lilikuwa la kweli.
Eliana alisimama kwa sekunde kadhaa akimtazama.
"Yule ni nani?" aliuliza.
"Mfanyakazi mpya wa shambani."
"Hajaitwa?"
"Daniel."
Hakusema tena.
Lakini tangu siku hiyo, macho yake yalikuwa yanamtafuta kila alipokuwa bustanini.
Siku moja alimkuta Daniel akimwagilia maua.
"Habari."
Daniel alishtuka.
"Nzuri dada."
"Usiniite dada."
Daniel alinyamaza.
"Basi niite Eliana."
"Samahani... siwezi."
"Kwa nini?"
"Wewe ni binti wa tajiri."
Eliana alitabasamu.
"Na wewe ni binadamu kama mimi."
Maneno hayo yalibaki moyoni mwa Daniel.
Kuanzia siku hiyo wakaanza kuzungumza mara kwa mara.
🔒
Endelea kusoma hadithi hii
Umesoma sehemu 3 za bure. Ili kumaliza hadithi hii, jiunge usome zote kwa TZS 2,000 / wiki au nunua hadithi hii tu kwa TZS 1,200.
Tayari una akaunti? Ingia
Zaidi katika Mapenzi
Kijana wa Shamba na Binti wa Tajiri
Juma alikuwa maskini asiye na kitu ila mikono yake na moyo wa unyenyekevu. Aliajiriwa kama kijana wa shamba kwa Bwana Mtenga — hakujua kwamba binti wa pekee wa tajiri, Zawadi, angempenda kwa mtazamo wa kwanza. Penzi lililokatazwa, ujauzito, kutoroka usiku wa dhoruba… na safari ndefu kutoka shambani hadi kileleni cha utajiri.
Mvua ya Novemba
Zainabu hakuwahi kuipenda mvua. Lakini mchana mmoja wa Novemba, akiwa amekwama chini ya paa la duka pale Posta, mvua ilimletea kitu ambacho hakukitegemea maishani mwake…
Barua Toka Zanzibar
Kila mwaka, tarehe kumi na tano Julai, Halima hufungua kasha dogo la mbao lililojaa barua za zamani. Ndani yake kuna mapenzi yaliyotenganishwa na bahari — na barua moja iliyochelewa miaka ishirini…
Ahadi ya Mwezi Mpevu
Chini ya mwezi mpevu, vijana wawili waliapiana ahadi ambayo dunia iliahidi kuivunja. Amina aliozwa kwa tajiri; Faraji akaondoka na ufukara wake. Lakini kila mwezi ulipopevuka, ahadi ile iliwaita…
Maoni
💬
Maoni ni kwa wanachama
Jiunge na Kurasa ili uweze kushiriki mawazo yako na kujadili hadithi pamoja na wasomaji wengine.
Tayari una akaunti? Ingia
Bado hakuna maoni. Kuwa wa kwanza kuandika!